Friday, March 30, 2012

Luteni Ligubi awaasa wananchi Hanang'

Afya ya Akili 
Ni katika maadhimisho ya Afya ya Akili yaliyofanyika mnamo katikati ya mwezi Machi mwaka huu katika hospitali  ya  wilaya ya Hanang’, inayojulikana kwa jina la Tumaini, ambapo mkuu wa wilaya ya Hanang, Mh. Luteni Ligubi aliwahusia wananchi wa wilaya  hiyo ya Hanang’ juu ya umuhimu wa afya ya akili.
Mh. Ltn Ligubi, Picha na Goustone Isole
Akizungumza mbele ya maafisa wengine mbalimbali, viongozi wa nyadhifa za juu wilayani hapo, watumishi wa hospitali hiyo pamoja na baadhi ya wananchi wa hapo, Mh. Luteni Ligubi amesema wilaya ya Hanang pamoja na wananchi wake kwa sasa iko katika hatari kubwa na watumiaji wa madawa ya kulevya kutokana na ukweli kwamba sekta ya usafirishaji kupitia wilaya hiyo imerahis
ishwa kutokana na kuwepo kwa barabara yenye ubora wa kiwango cha lami inayotazamiwa kukamilika ujenzi wake katikati ya mwezi Mei mwaka huu hivyo uingizaji wa haramu wa madawa ya kulevya utakuwa ni jambo lisilozuilika kama wananchi hawatatoa ushirikiano wa kutosha hususani kwa chombo cha usalama, jeshi la polisi.
Kikundi cha sanaa, Katesh
Mkuu huyo wa wilaya alitoa hamasa kwa waratibu wa afya ya akili katika hospitali hiyo ya wilaya kuandaa matamasha yanayokusudia kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa afya ya akili. Akizungumza kama mgeni wa rasmi, Mh. Luteni Ligubi alitanabanisha kwamba madhara yatokanayo na uharibifu wa afya ya akili ni pamoja na kuongezeka kwa matukio ya uhalifu katika jamii, wimbi la umaskini katika ngazi zote kuanzia familia hadi Taifa pamoja na maambukizi ya magonjwa hususani yale ya zinaa.
Aidha mkuu huyo wa wilaya alichukua nafasi hiyo pia kukichangia kikundi cha sanaa ya maigizo na nyimbo kinachojulikana kama ‘Upendo Group’ kiasi cha pesa taslimu shilingi laki moja ikiwa ni kama sehemu ya mchangokutoka ofisi yake ili kukiendeleza kikundi hicho ambacho pia kilikuwa kikihamasisha wananchi wakati wa tamasha hilo.
Naye mratibu mratibu wa afya ya akili katika hospitali hiyo, Bw. Tluway, alitamka kuwa idara yake itakuwa ikiandaa matamasha ya mara kwa mara katika mikusanyiko ya watu kwa ajili ya kuhamasisha afya ya akili.
Bw. Goustone Isole







Kuwasiliana na mwandishi wa Blog hii, Bw. Goustone  Isole
Tumia mawasiliano yanayoonekana kwenye kurasa tofauti na hii ndani ya Blog.

No comments:

Pageviews past week