Saturday, March 24, 2012

Mapenzi na Mahusiano


Na Goustone Isole 
Kila kukicha mapenzi katika maisha ya mwanadamu yamekuwa yakichukua nafasi kubwa ukiacha suala la kutafuta hela au mambo mengine yahusianayo na maendeleo.
Kutokana na hilo, nachukua nafasi hii, mimi kama mmoja wa wakereketwa wa suala la mapenzi, kuelezea kwa undani mambo muhimu ya kuzingatia katika mahusiano.
Wapenzi wenye furaha
Imekuwa ni kwa kawaida kwa mtu yeyote kusikika akisema eti mapenzi ya kweli hayaangalii pesa au mali…. hii naikataa tena kwa asilimia zote!! Kwa utafiti mdogo nilioufanya kwa muda usiopungua miaka minne…  nimegundua kwamba wengi wanaojinadi kuwa mapenzi hayaangalii kipato ni wale ambao hujiingiza kwenye mahusiano na wapenzi zaidi ya mmoja…   hii ikimaanisha kuwa mmoja/ wengineo ni wa kujipatia kipato na mwingine ni wa kuridhisha moyo wake kwa kuwa ndiye anayempenda kwa moyo wake wote ila kwa sababu ya yeye kuwa na kipato kidogo basi anakuwa hana budi kufanya kile ambacho kitamsaidia katika dunia hii ya Sayansi na Teknolojia. Hii pia hutokea kwa wanaume wapenda vya bure.
Ukweli ni kwamba hakuna binadamu yeyote apendaye maisha mabaya….. na tutambue katika maisha yetu ya kila siku tangu enzi na enzi tena zile za Adam na Hawa, mwanaume aliumbwa mtafutaji na mwamuzi wa mambo mengi katika maisha ya kila siku iwe ni katika nyanja ya kijamii, kiuchumi au hata kisiasa. Cha ajabu kutokana na  utandawazi basi siku hizi wanawake na wao wanajiweka mstari wa mbele kudai haki ya kuwa na maamuzi katika nyanja zote zilizozibainisha hapo awali. Kama matokeo yake, leo si ajabu kuona mwanamke ameoa mwanaume, na yeye mwanamke kuwajibika kwa kila hali kuhakikisha mwanaume anafurahi kama ambavyo wanaume wengi wapendavyo kuhakikisha  wanawafurahisha wapenzi wao kwa kuwapa yale wanayohisi ni bora zaidi… Mbaya zaidi ikitokea kwamba mwanaume akashindwa kumfurahisha mpenzi wake ni kawaida kwa mwanaume kuleta visingizo vya hapa na pale ili mradi tu aachane na mwenzi wake yote ili kuepusha fedheha ya kushindwa kuonesha udume wake!!! Kwa mfano huo hafifu nadhani ntakuwa nimeeleweka kuwa Mahusiano na Uwezo ni vitu ambavyo vinaenda kwa pamoja….
Wapenzi wakijadiliana jambo
Itakuwa ni jambo la busara kukumbushia makala moja maarufu kama Wanawake Live inayorushwa hewani na chaneli maarufu ya East AfricaTv ama Chanel 5 mwanzoni mwa mwezi Machi..  hii ilihusu ni mambo gani hupeleka mwanaume kukataliwa na wazazi wa msichana pindi linapokuja swala la wawili hao kutaka kuishi pamoja kama Mume na Mke!!
Wachangia mada waliweka bayana kwa kuonesha kuwa ni rahisi kwa mwanaume kukubalika kwa upande wa binti kama tu atakuwa na mambo yafuatayo
  • ·         Elimu ya kutosha angalau hata Shahada moja ikiwa ni imani ya wazazi kuwa mwanaume mwenye Elimu ana uelewa mpana na hivyo inakuwa ni rahisi katika suala zima la kupambana na maisha.
  • ·         Pia ni imani kuwa huwa ni sifa kwa wazazi wa binti kuona binti yao ameolewa na watu wafanyao kazi za sifa kubwa kama vile Madaktari au wanasheria.
Pamoja na kuweka hoja hii wazi, sijamaanisha eti wazazi basi wawachagulie mabinti zao au hata vijana wao wenza … Hiyo sitaki kusikia hata kidogo!! Vijana mna haki katika masuala ya mahusiano katika kuchagua mwenza, nafasi ya mzazi au mlezi ni kushauri tu na kufundisha namna ya kuishi maisha ya wawili (Ndoa).
Niwatakie maisha mema vijana wa leo au wazee wa kesho hasa ya Mahusiano….

Wenu katika Kuelimishana, Kaka Goustone Isole                                                                                

No comments:

Pageviews past week